WELCOME TO TSC OFFICIAL BLOG: CONTACT US: Phone Numbers: +255-26- Or +255-26- Fax Numbers: +255-26- Or +255-26-, E-MAIL: secretary@tsc.go.tz.

Monday, January 23, 2017

Mhe. George B. Simbachawene awapisha wajumbe wa Bodi ya Tume ya Utumishi wa Walimu

Mkurugenzi wa Tume ya Utumishi wa Waalimu (TSC) Bw. Erasmus Rugarabamu akimkaribisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI TAMISEMI Mhe. George B. Simbachawene (Mb) kutoa hotuba ya Ufunguzi wa kikao cha kazi cha Tume ya Utumishi ya Waalimu (Teachers Service Commission – TSC) katika ukumbi wa Taifa wa kuhifadhia nyaraka mjini Dodoma. Waliokaa katikati ni Waziri wa Nchi TAMISEMI, kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume TSC Bw. Oliva Mhaiki na kulia kwake ni Katibu wa Tume ya Walimu (TSC) Bi. Winfrida Rutaindurwa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI TAMISEMI Mhe. George B. Simbachawene (Mb) akitoa hotuba ya Ufunguzi wa kikao cha kazi cha Tume ya Utumishi ya Waalimu (Teachers Service Commission – TSC) katika ukumbi wa Taifa wa kuhifadhia nyaraka mjini Dodoma



Bw. Costantine Machoko akiapa mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George B. Simbachawene (Mb) kuwa mjumbe wa Bodi ya Tume ya Utumishi ya Walimu (TSC) katika ukumbi wa Taifa wa kuhifadhia nyaraka mjini Dodoma. Waliosimama kulia kwake ni Mkurugenzi wa TSC Bw. Erasmus Rugarabamu na Katibu wa Tume ya Walimu (TSC) Bi. Winfrida Rutaindurwa.
  

Bw. Ramadhani Samainda akiapa mbele ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. George B. Simbachawene (Mb) kuwa mjumbe wa Bodi ya Tume ya Utumishi ya Walimu (TSC) katika ukumbi wa Taifa wa kuhifadhia nyaraka mjini Dodoma. Waliosimama kulia kwake ni Mkurugenzi wa TSC Bw. Erasmus Rugarabamu na Katibu wa Tume ya Walimu (TSC) Bi. Winfrida Rutaindurwa






Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI TAMISEMI Mhe. George B. Simbachawene (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Walimu (TSC) na baadhi ya Wakurugenzi wa TSC waliokaa kulia kwake ni Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu Bw. Oliva Mhaiki na kushoto kwake ni Katibu wa Tume ya TSC Bi. Winfrida Rutaindurwa.





Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. George Simbachawene (Mb) ameitaka Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) kufanya kazi  kwa uadilifu na uaminifu ili  kufanikisha ufanisi  na kuepuka udanganyifu katika utendaji  wake.
Mhe.  George B. Simbachawene (Mb)   aliyasema hayo katika kikao kazi  cha chombo hicho kilichoambatana na kuapishwa kwa wajumbe wapya wawili   katika ukumbi wa Nyaraka za Taifa  Dodoma hapo jana ambapo aliwataka watendaji wa Tume hiyo kufanya kazi kwa uweledi mkubwa  ili kufikia malengo ya Tume na  kukidhi haja ya wananchi kwa ujumla.
Mhe. Waziri  aliongeza kuwa  matarajio ya chombo hiki ni kikubwa hivyo  watendaji wanatakiwa kutekeleza majukumu yao  yakiwemo kuendeleza na kusimamia utumishi wa walimu, kuajiri  kupandisha vyeo na kuchukua hatua za kinidhamu  kwa walimu na kumshauri waziri mwenye dhamana  na Serikali za  mitaa masuala mbalimbali yanahusiana na Tume hiyo.
“ Katika sheria ya Mwaka 2015  kifungu namba 5 kimeainisha majukumu ya chombo hiki ,  matarajio ya Serikali na Wananchi ndio yaliyofanya kuanzishwa kwa chombo hiki na kimepewa dhamana kubwa kustawisha sekta ya elimu na kupaza sauti kwa niaba ya walimu ” alibainisha Mhe.Simbachawene
Aidha Mhe. Waziri alieleza kuwa Tume hii ni chombo cha haki ili kufanya kazi kwa umakini  lazima watendaji wawe waadilifu kuanzia kwenye ngazi ya wilaya  ambao watakaoenda  sambamba na mabadiliko ya sekta ya elimu na kama hawatenda haki  basi chombo hiki kitashindwa kutimiza majukumu yake ambayo yatafanywa na vyombo vingine rasmi au sio rasmi .
Pia aliwataka wajumbe na watendaji wote kuwa makini katika mada zote zinazowasilishwa katika kikao kazi hicho ili kuendeleza uweledi walinao  utakaofanikisha utendaji kazi wa Tume hiyo na kuhakikisha  kazi inafanyika bila udanganyifu na upendeleo wowote .
Kwaupande wake  Costantine Mashoko ambaye ni mjumbe wa Tume hiyo amehaidi kuwa  wajumbe watashirikiana na sekretarieti , mwenyekiti , katibu wa Tume  pamoja  na wadau mbalimbali wa elimu  ili kutekeleza majukumu kwa   uweledi  na kuhaidi kuteua watendaji waaminifu   ngazi ya wilaya watakaotenda kazi kwa haki.

No comments:

Post a Comment